Pages

Tarumbeta Banner

Monday, February 27, 2012

Mayai ‘feki’ yatua Dar

AFYA za Watanzania zipo hatarini kutomkana na kuingizwa nchini kwa mayai feki, Mwananchi Jumapili limebaini. Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili na kuthibitishwa na wafanyabiashara nchini, umebaini kuwa soko la Dar es Salaam limevamiwa na mayayi hayo yaliyoingizwa nchini kutoka Kenya na yanauzwa kwa bei rahisi huku ubora wake ukitiliwa mashaka.

Kwa mujibu wa maelezo ya wafanyab iashara hao, mayai hayo huuzwa Sh4,000 kwa trei na yanaonekana sio makubwa kama yanayopatikana nchini na yanapovunjwa hayana kiini na baadhi maji yake yamechanganyika na vitu mithili ya nyuzi zenye rangi nyekundu.

Wafanyabiashara hao wanalalamika kuwa kuingizwa nchini kwa mayai hayo yamevuruga soko la ndani ambalo trei moja ilikuwa inauzwa kwa Sh7,000 lakini hayo yanauzwa Sh4,000.

Mayai hayo yanapatikana kwa wingi maeneo ya Kariakoo na Gongo la Mboto na yanauzwa kwa wingi kwa wafanyabiashara wa vyakula jijini Dar es Salaam. Akizungumza na gazeti hili, Mwenyekiti wa Muda wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Mayai Tanzania, Placidia Bambanza alisema mayai hayo yalianza kuingia nchini tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

“Tumepanga kupeleka malalamiko yetu kesho (jumatatu) kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na tayari tumeandaa baadhi ya mayai hayo tumuonyeshe na atambue ubovu wake,” alisema Bambanza.

Alisema kuwa hali hiyo imewafanya nao waanze kuuza mayai kwa Sh5000 badala ya Sh7000, jambo ambalo alisema kuwa linawafanya wapate hasara kubwa.
“Tuligundua kuwa mayai haya yanatoka Kenya kwa kuwa wateja wetu ambao awali tulikuwa tukiwauzia mayai, hivi sasa hawanunui kwetu na wanatueleza kuwa wananunua mayai hayo kwa wafanyabiashara kutoka Kenya,” Aliongeza, “Wanatueleza wazi kuwa mayai hayo yanauzika kwa wafanyabiashara wa vyakula kwa kuwa si rahisi kuonekana na watumiaji kama yana kasoro, ila kwa watu ambao hununua mayai kwa ajili ya kuwauzia watu wengine, huyakataa mayai hayo kwa sababu hayauziki na baadhi ya watu wameanza kuyagundua hayafai.”

Alisisitiza kuwa uingizwaji wa mayai hayo nchini unawapa wakati mgumu kwa kuwa wengi wao wamechukua mikopo katika benki mbalimbali nchini, hivyo kitendo cha kuuza trei moja kwa Sh 5000 kinawafanya wapate hasara. Mmoja wa wafanyabiasha hao, Mseti Marwa alisema; “Kama serikali imeruhusu mayai haya yaingie nchini basi wote tuuze bei moja, pia kama wafanyabiashara hawa wana kibali cha kuuza bidhaa hii basi serikali inatakiwa kushusha viwango vya bei za vyakula vya kuku na dawa ili tuweze kuuza kwa bei inayofanana”.

Katika hatua nyingine wafanyabishara hao walilalamikia kampuni za kuuza vifaranga nchini kutokana na vifaranga hivyo kutokuwa na ubora unaotakiwa. “Unaweza kukuta unanunua vifaranga 500 lakini vinatoa mayai trei nane hadi saba tu kitu ambacho si cha kawaida…, katika malalamiko yetu tutaitaka serikali ituruhusu tununue vifaranga kutoka nje ya nchi,” alisema Bambanza Kauli ya serikali Akizungumzia suala hilo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo alisema kuwa yuko tayari kuyapokea malalamiko ya wafanyabiashara hao na kuyafanyia kazi.

“Hilo jambo ndio kwanza nalisikia kutoka kwao… Ila serikali ipo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa soko la ndani linaimarika hivyo nawasubiri ili nisikilize malalamiko yao na nitayafanyia kazi,” alisema Dk Mathayo. Akizungumzia suala la wafanyabiashara kununua vifaranga nje ya nchi alisema, “Wanaweza kufanya hivyo ila ni mpaka wapate vibal.”

No comments:

Post a Comment