LONDON, England
KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amempongeza mkongwe wake, Ryan Giggs akisema ni kati ya wachezaji wanaozeeka huku kiwango cha soka kikiwa bado juu.
Giggs, 38, ambaye amecheza mechi 900 za United kaika mashindano yote, ni kati ya wachezaji wanaotarajiwa kupewa heshima katika klabu hiyo kwa utumishi wa muda mrefu.
Hiyo itamfanya Giggs kuendelea kuuwania ubingwa ikiwa ni pamoja na kuwa miongoni mwa wachezaji wa pambano la Norwich lililopigwa jana na Ferguson anaamini kuwa hakuna mchezaji kama yeye.
"Kwa mtazamo wangu, na siamini kama kila mmoja atakubaliana na mimi, kuwemo kwenye Ligi Kuu na licha ya kufaya makubwa, siamini kama kuna mchezaji mwingine anaweza kumfikia," anasema kocha wa United juzi.
"Pamoja na ukongwe wake, anajaribu kutengeneza mazingira mazuri kufanikisha azma ya uchezaji wake. Anacheza kiwango cha juu, na leo, anacheza kama wachezaji wengine. Anafurahisha."
Ferguson anaamini kuwa kujituma, kujitunza na kufuata taratibu za mchezo ndicho kilichomfanya Giggs kucheza kwa muda mrefu.
"Giggs ni kati ya wachezaji waliokomaa, amekuwa akikimbiza vizuri na zaidi hupenda kusimama namba za katikati ya dimba la mbele. Huopewa nafasi kama mchezaji wa kipekee kwenye timu," anasema.
"Itakumbukwa Ryan a mekuwa mchezaji mashuhuri kwa kupanda na kushuka na mch ezaji makini sana anapokuwa uwanjani.
"Amekuwa akibadilika sana na amekuwa akibadilika tofauti na ilivyokuwa miaka 10 iliyopita na anapokuwa mchezoni anaonekana tofauti na unavyomdhania."
Giggs ameingia mkataba wa mwaka mmoja, utakaomfanya abaki Old Trafford hadi mwisho wa msimu wa 2013 na, pia amecheza mechi 64 na timu ya taifa ya Wales na mbili za U-21 na lengo lake ni kufikisha mechi 1,000 kabla ya kustaafu soka.
"Juu ya umri," Ferguson, anasema kuwa hilo linawezekana.
"Stanley Matthews amecheza soka akiwa na miaka 50, tusubiri kwa Giggs na tuone."
*Maisha ya Giggs
Ryan Joseph Wilson ni mtoto wa kufikia aliyelelewa katika kituo cha St David's Hospital mjini Canton, Cardiff, cha Danny Wilson,
Akiwa na umri mdogo Giggs amekulia katika eneo la Ely, magharibi mwa Cardiff. Mdogo wake, Rhodri, alikuwa akiichezea klabu ya Salford City.
Ametumia muda mwingi kucheza barabarani na watoto wenzake kwenye mji wa Pentrebane. Mwaka 1980, Giggs akiwa na miaka sita, alisaini Swinton RLFC, na familia nzima ikahamia Swinton, katika mji wa Salford, Greater Manchester.
Mwaka 1990-1995, alianza kuichezea Manchesster United kwani alipewa mkataba Novemba 29, 1990 (akiwa na miaka 17). Alianza kucheza soka kama mwanasoka wa kulipwa (1 Desemba 1990).
Akiwa na timu hiyo kombe lake la kwanza lilikuwa FA na kimsingi Giggs alianza kuichezea timu yake dhidi ya Everton kwenye Uwanja wa Old Trafford Machi 2, 1991 akitokea benchi kuchukua nafasi ya Denis Irwin.
Giggs alianza kuichezea timu ya kwanza akiwa na miaka 17, na kuweka rekodi yake kuwa mchezaji mwenye umri mdogo kuitumikia Manchester United. Huo ukawa mwanzo wa kuitumikia klabu ya wakubwa ya Ferguson

No comments:
Post a Comment