LONDON, England
CHELSEA imeendelea kuchanja mbuga baada ya kuibandua Bolton mabao 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya England na kumaliza ukame wa ushindi wa timu hiyo wa mechi tano mfululizo.
Bolton iliyokuwa imeikaba Blues lakini kabla ya mapumziko, Mbrazil, David Luiz alitupia mpira ndani ya kimia kuandika bao la kwanza kwa timu yake.
Didier Drogba alipiga kichwa cha karibu na kufanya matokeo kuwa 2-0 kabla ya Frank Lampard kumalizia krosi ya Juan Mata.
Wageni walipoteza nafasi baada ya Ryo Miyaichi kukosa bao la wazi ambalo lingewafanya kuwa mbele kabla ya Chelsea kufunga. Chelsea imefikisha pointi 46 na kuishusha Arsenal ambayo jana ilikuwa na kazi dhidi ya Tottenham.
Mechi nyingine za jana usiku, Norwich ilikuwa ikicheza na Man United huku Stoke ikiikaribisha Swansea.
Mbali na mechi hizo, West Brom iliyokuwa nyumbani hiyo juzi, iliitandika Sunderland mabao 4-0. Sunderland iliifunga Arsenal katika moja ya mechi za ligi hiyo hivi karibuni.
Nayo QPR ilishindwa kutumia uwanja wa nyumbani na kuchapwa bao 1-0 na Fulham wakati Newcastle ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 2-2 na Wolves. Wigan na Aston Villa zenyewe zilitoka suluhu katika mfululizo wa mechi hizo.

No comments:
Post a Comment