LONDON, England
WIKI mbili zilizopita, zilikuwa mbaya kwa mashabiki wa Arsenal. Katika kipindi cha siku nne, the Gunners ilichapwa na AC Milan 4-0, na kuififisha nafasi ya Arsenal kuendelea na Ligi ya Mabingwa Ulaya. Na Jumamosi Februari, 18, Sunderland iliwaliza Gunners 2-0.
Kwa hali hiyo, inafanya kikosi cha Arsene Wenger kumaliza msimu wa saba bila ubingwa na zaidi ni baada ya kufungwa mechi ya Sunderland.
Arsenal inatakiwa kufanya mabadiliko makubwa na zaidi katika kutengeneza kikosi cha kwanza kwanza. Kwa mujibu wa Sunday Mirror, miongoni mwa watu wa ngazi za juu wa Gunners kuna haja ya kufanyia mabadiliko safu nzima ya timu.
Manchester City imeanza kuiga staili ya Arsenal kwani imeanza kutengeneza wachezaji chipukizi. Cha kushangaza, Wenger na uongozi mzima wa Arsenal wanashindwa kutoka kupitia mazao ya chipukizi wao.
Mpango wa sasa ni kumpatia Wenger uwezo wa kusajili wachezaji wakubwa na kuongeza mishahara kwa wachezaji waliopo, Robin van Persie, Arsenal ni miongoni mwa wachezaji watakaoneemeka.
Robin van Persie amebakisha mwaka mmoja kumaliza mkataba wake na Arsenal. Bosi ya klabu kwa sasa inazungumza na Wenger kwa ajili ya kununua wachezaji wakubwa kuibeba klabu.
Baadhi wameanza kusema kuwa hali ni mbaya kwa sasa Arsenal katika historia ya uongozi wake na kwamba mechi mbili zilizopita, zimekuwa tatizo.
Ni wakati kwa Arsenal kufanya maamuzi magumu. Inatakiwa kutengeneza timu kutoka uwanjani hadi kwa wachezaji mmoja mmoja kwani vinginevyo mashabiki wanaweza wasinunue ama kubakia vyooni wakiangalia kupitia kwenye televisheni.

No comments:
Post a Comment