![]() | |
| Bongo Talents Alive (BTA) Wakiwa kwenye pozi |
Friday, August 3, 2012
Bongo talents alive ndani ya Bukoba
Friday, April 27, 2012
JK aitisha Kamati Kuu CCM ghafla!
NI KUJADILI MUSTAKABALI WA MAWAZIRI WALIOTAKIWA KUJIUZULU, WENYEWE WAVUNJA UKIMYA
Waandishi Wetu
WAKATI joto la wabunge, vyama vya siasa na wanaharakati nchini kutaka mawaziri waliohusishwa na kashfa kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wajiuzuluzu likizidi kupanda, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete ameitisha kikao cha ghafla cha Kamati Kuu ya chama hicho kujadili pamoja na mambo mengine, hali ya siasa nchini.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, zilieleza kuwa kikao hicho kitafanyika leo Ikulu ya Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Ingawa Nape alisema hawezi kutaja ajenda za kikao hicho kwa kuwa ni siri, habari kutoka baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, zilidokeza kuwa hakuna namna, Rais Kikwete akakwepa kuzungumzia shinikizo la mawaziri hao kujiuzulu.
"Ni kweli kesho (leo) tuna Kamati Kuu Dar es Salaam, lakini agenda za kikao hicho haziwezi kuwekwa 'public' ujue hivyo tu inatosha," alisema Nape.
Nape alishindwa kuthibitisha au kukanusha taarifa kwamba kikao hicho kitajadili hatima ya mawaziri hao wanaotakiwa kujiuzulu badala yake akasema,"Kama nilivyokwambia hakuna agenda ya kuweka 'public' wewe hayo unayoyazungumza unayajua wewe ukitaka yangu, andika nilichokwambia."
Mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu ni Kepteni George Mkuchika (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Tamisemi), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), William Ngeleja (Nishati na Madini), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Profesa Jumanne Maghembe (Kilimo, Chakula na Ushirika), Mhandisi Omar Nundu (Uchukuzi) pamoja na Mkulo na Nyalandu.
Wakati kukiwa na taarifa za Kamati Kuu kuwajadili mawaziri hao, watano kati yao wameonekana kutokuwa tayari kujiuzulu huku baadhi wakihoji sababu za kufanya hivyo na Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo akisema kuwa hajui madai ya wabunge hao dhidi yake.
Waziri Mkulo (Fedha), Lazaro Nyalandu (Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko) na Athuman Mfutakamba (Naibu Waziri wa Uchukuzi), walisema hawafikirii kujiuzulu kwa kuwa hawajui makosa yao.
Shinikizo la kutaka mawaziri nane wajiuzulu liliibuka katika Mkutano wa Saba wa Bunge uliomalizika mjini Dodoma mwanzoni mwa wiki hii, baada ya ripoti hiyo ya CAG kuonyesha tuhuma nzito za ufisadi katika wizara hizo huku baadhi ya mawaziri wakionekana kuhusika moja kwa moja na maamuzi waliyofanya.
Baadhi ya mawaziri hao walitoa utetezi wao bungeni na wengine walipokutana kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari, lakini jitihada hizo za kujisafisha hazikuzaa matunda kutokana na ongezeko la shinikizo hilo kutoka kwa makundi mbalimbali ya kijamii.
Mkulo: Sijui kinachoendelea
Mkulo ambaye alikuwa waziri wa kwanza kutakiwa na wabunge ajiuzulu, kutokana na kashfa ya kuvunja Bodi ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) ili kuficha tuhuma zake ikiwemo uuzaji wa kiwanja Na.10 kwa Kampuni ya Mohamed Enterprises (MeTL), alisema hawezi kuzungumzia suala la kujiuzulu kwa sababu hajui kosa lake wala madai ya wabunge dhidi yake.
Waziri huyo alisema yaliyozungumzwa na wabunge hakuyasikia kwa kuwa hakuwapo bungeni Dodoma kwa muda mrefu kutokana na kuwa safarini.
Alipoulizwa kama yuko tayari kujiuzulu kuhusiana na kashfa zinazoikabili wizara yake, Mkulo alijibu, ‘ hapa, no comment," akiwa na maana kwamba hana cha kuzungumza.
“Kwanza sifahamu tuhuma zilizotolewa na wabunge kwa sababu sikuwepo, mimi nilikuwa safari,” alisema.
Hata alipoulizwa kuhusiana na wizara yake kuuza kiwanja hicho cha Serikali kilichopo katika Barabara ya Nyerere, jijini Dar es Salaam kinyume cha taratibu, Mkulo aliendelea kusema, ‘no comment, no comment kwa hilo.’
Mfutakamba
Jana Mfutakamba aliliambia Mwananchi kuwa haoni sababu yoyote ya kujiuzulu kwani hana tuhuma zozote ndiyo maana pia hata wabunge katika orodha yao hawakuweza kumtaja popote.
Mfutakamba alitoa kauli hiyo wakati ambao Waziri Nundu amemtuhumu kwamba amekuwa akishinikiza Kampuni ya China Communication Construction Company (CCCC), ipewe kazi ya kujenga gati namba 13 na 14 katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuwa ilimgharamia safari kwenda nje ya nchi.
Hata hivyo, Mfutakamba alikiri kusafirishwa na kampuni hiyo na kuongeza kwamba alikwenda huko kutembelea miradi mbalimbali ikiwamo ya ujenzi wa reli na magati kwa kufuata taratibu zote na aliporudi aliieleza Serikali uwezo wa kampuni ya CCCC, Kampuni ambayo inapingwa na Nundu aliyedai kuwa ilimsafirisha Mfutakamba baada ya yeye kukataa.
Nyalandu
Jana, Nyalandu alisema kuwa, mpaka sasa haelewi kwanini ameingizwa kwenye kashfa hiyo kwa sababu katika ripoti ya CAG, hakutajwa na wenyeviti wa kamati mbalimbali za kumudu za Bunge.
“Sielewi kwanini nimeingizwa kwenye kashfa hii kwa sababu katika ripoti ya CAG sikuwemo. Ripoti ya Mwenyekiti wa Kamati ya POAC na PAC simo pia, lakini nilishangaa nilipoanza kusikia jina langu,” alisema Nyalandu.
Aliongeza kuwa baadhi ya mawaziri waliotuhumiwa kwenye kashfa hiyo waliitwa na Kamati ya CCM kwa ajili ya mahojiano, lakini yeye hakuitwa.
Alisema kutokana na hali hiyo anashindwa kuelewa kwanini jina lake lilikuwa miongoni mwa watu waliotajwa wakati hayumo kwenye ripoti yoyote.
Alisema kutokana na hali hiyo anaamini kuwa watu waliomtaja wana sababu zao binafsi, kwamba Kamati za Bunge ndizo zenye majukumu ya kuthibitisha ukweli kuhusu tuhuma anazopewa.
Tayari Nyalandu alitoa waraka unaonyesha msimamo tofauti na wa bosi wake, Dk Chami kuhusu kashfa zinazowakabili ambazo ni tuhuma alizonazo Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Viwango (TBS), Charles Ekelege anayedaiwa kuanzisha kampuni hewa za ukaguzi wa magari nje ya nchi hususani, Hong Kong na Singapore.
Wakati Nyalandu akishauri Ekelege asimamishwe kazi ili apishe uchunguzi wa CAG na endapo hatakuwa na tuhuma za kujibu arudishwe kazini, waziri wake (Chami) alisema kuwa Ekelege ni mteule wa rais, hivyo hawezi kwenda kwa Rais Jakaya Kikwete kumtaka amwondoe wakati hakuna taarifa yoyote inayoonyesha tuhuma zake.
Sakata la kuwepo kwa kampuni hizo hewa za ukaguzi wa magari liliwekwa wazi katika ripoti iliyotolewa na CAG na wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) inayoongozwa na Zitto Kabwe na ile ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC) ya John Momose Cheyo huku ikielezwa kuwa wanamkingia kifua Ekelege kutokana na kushindwa kumchukulia hatua.
Mponda aahidi kuweka mambo hadharani leo
Kwa upande wake, Dk Mponda alipoulizwa kama atajiuzulu kutokana na kashfa zinazoikumba wizara yake alisema atazungumzia suala hilo kesho (leo) na kuongeza, “Njoo Ijumaa tutazungumza, leo sisemi chochote, nipigie asubuhi ili nikupangie muda wa kuja ofisini,”alisema Dk Mponda.
Waziri huyo anakabiliwa na kashfa ya Bohari ya Dawa (MSD) ambako ukaguzi maalum katika bohari hiyo uliofanyika ulibaini kuwapo tofauti ya Sh 658.9 milioni ikiwa ni pungufu ya kiasi ambacho kilipokelewa na kuripotiwa wizarani kwenda MSD, huku ushahidi wa kuzipokea kutotolewa.
Pia, uchunguzi unaonyesha kuwapo Sh 100 milioni zilizopelekwa MSD kutoka Wizara ya Afya na kutumiwa na bohari hiyo bila kuwepo kwa mchanganuo wa matumizi.
Ukaguzi pia ulibaini kuwepo kwa kiasi cha Sh 4.5 bilioni zilizotoka Hazina kwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kununulia dawa na vifaa vya hospitali, lakini kiasi cha Sh 4.344 bilioni ndio kilichopelekwa MSD ukiondoa Sh 196 milioni ambazo zilitumika bila kuwapo kwa ushahidi wa kupokelewa MSD kutoka Wizara ya Afya.
Maige anena
Waziri Maige juzi aliamua kueleza baadhi ya tuhuma zinazomkabili ikiwamo umiliki wa nyumba aliyodaiwa kuinunua kwa Dola 700,000 za Marekani, akisema nyumba hiyo aliinunua kwa dola 410,000 na siyo dola 700,000 kama ilivyoelezwa.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Malisili na Mazingira, James Lembeli alipinga kauli hiyo akisema taarifa alizonazo zinaonyesha Maige alinunua nyumba hiyo kwa fedha taslimu dola 700,000.
Kashfa nyingine inayomkabili Maige ni ile iliyotolewa na Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira huku ikitaka awajibishwe kwa kutengeneza mazingira ya rushwa katika ugawaji wa vitalu vya uwindaji kwa kampuni ambazo hazina sifa na kusafitishwa nje kwa wanyama wakiwamo twiga na tembo kinyume cha sheria.
Hata hivyo, Maige alisema hivi sasa kuna mapambano ya kisiasa baina ya viongozi mbalimbali na kwamba habari mbaya dhidi yake zinalenga kumchafua kutokana na kuwa mkali katika utendaji wake wa kazi na kuongeza, kuna chuki kutokana na kwamba aliwahi kuwafukuza kazi baadhi ya watendaji wizarani kwake jambo ambalo limewaudhi baadhi yao.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) Zitto Kabwe ndiye aliyenogesha hoja hiyo ya kutaka mawaziri hao wajiuzulu baada ya kutaka Bunge lipige kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kama Serikali haitawafukuza kazi mawaziri hao.
*Habari hii imeandaliwa na Raymond Kaminyoge, Patricia Kimelemeta, Aidan Mhando na Fidelis Butahe
Habari kutoka:
http://www.mwananchi.co.tz/component/content/article/37-tanzania-top-news-story/22385-jk-aitisha-kamati-kuu-ccm-ghafla.html
Tuesday, April 10, 2012
Tuesday, March 6, 2012
Monday, February 27, 2012
Mayai ‘feki’ yatua Dar
AFYA za Watanzania zipo hatarini kutomkana na kuingizwa nchini kwa mayai feki, Mwananchi Jumapili limebaini. Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili na kuthibitishwa na wafanyabiashara nchini, umebaini kuwa soko la Dar es Salaam limevamiwa na mayayi hayo yaliyoingizwa nchini kutoka Kenya na yanauzwa kwa bei rahisi huku ubora wake ukitiliwa mashaka.
Kwa mujibu wa maelezo ya wafanyab iashara hao, mayai hayo huuzwa Sh4,000 kwa trei na yanaonekana sio makubwa kama yanayopatikana nchini na yanapovunjwa hayana kiini na baadhi maji yake yamechanganyika na vitu mithili ya nyuzi zenye rangi nyekundu.
Wafanyabiashara hao wanalalamika kuwa kuingizwa nchini kwa mayai hayo yamevuruga soko la ndani ambalo trei moja ilikuwa inauzwa kwa Sh7,000 lakini hayo yanauzwa Sh4,000.
Mayai hayo yanapatikana kwa wingi maeneo ya Kariakoo na Gongo la Mboto na yanauzwa kwa wingi kwa wafanyabiashara wa vyakula jijini Dar es Salaam. Akizungumza na gazeti hili, Mwenyekiti wa Muda wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Mayai Tanzania, Placidia Bambanza alisema mayai hayo yalianza kuingia nchini tangu mwanzoni mwa mwaka huu.
“Tumepanga kupeleka malalamiko yetu kesho (jumatatu) kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na tayari tumeandaa baadhi ya mayai hayo tumuonyeshe na atambue ubovu wake,” alisema Bambanza.
Alisema kuwa hali hiyo imewafanya nao waanze kuuza mayai kwa Sh5000 badala ya Sh7000, jambo ambalo alisema kuwa linawafanya wapate hasara kubwa.
“Tuligundua kuwa mayai haya yanatoka Kenya kwa kuwa wateja wetu ambao awali tulikuwa tukiwauzia mayai, hivi sasa hawanunui kwetu na wanatueleza kuwa wananunua mayai hayo kwa wafanyabiashara kutoka Kenya,” Aliongeza, “Wanatueleza wazi kuwa mayai hayo yanauzika kwa wafanyabiashara wa vyakula kwa kuwa si rahisi kuonekana na watumiaji kama yana kasoro, ila kwa watu ambao hununua mayai kwa ajili ya kuwauzia watu wengine, huyakataa mayai hayo kwa sababu hayauziki na baadhi ya watu wameanza kuyagundua hayafai.”
Alisisitiza kuwa uingizwaji wa mayai hayo nchini unawapa wakati mgumu kwa kuwa wengi wao wamechukua mikopo katika benki mbalimbali nchini, hivyo kitendo cha kuuza trei moja kwa Sh 5000 kinawafanya wapate hasara. Mmoja wa wafanyabiasha hao, Mseti Marwa alisema; “Kama serikali imeruhusu mayai haya yaingie nchini basi wote tuuze bei moja, pia kama wafanyabiashara hawa wana kibali cha kuuza bidhaa hii basi serikali inatakiwa kushusha viwango vya bei za vyakula vya kuku na dawa ili tuweze kuuza kwa bei inayofanana”.
Katika hatua nyingine wafanyabishara hao walilalamikia kampuni za kuuza vifaranga nchini kutokana na vifaranga hivyo kutokuwa na ubora unaotakiwa. “Unaweza kukuta unanunua vifaranga 500 lakini vinatoa mayai trei nane hadi saba tu kitu ambacho si cha kawaida…, katika malalamiko yetu tutaitaka serikali ituruhusu tununue vifaranga kutoka nje ya nchi,” alisema Bambanza Kauli ya serikali Akizungumzia suala hilo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo alisema kuwa yuko tayari kuyapokea malalamiko ya wafanyabiashara hao na kuyafanyia kazi.
“Hilo jambo ndio kwanza nalisikia kutoka kwao… Ila serikali ipo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa soko la ndani linaimarika hivyo nawasubiri ili nisikilize malalamiko yao na nitayafanyia kazi,” alisema Dk Mathayo. Akizungumzia suala la wafanyabiashara kununua vifaranga nje ya nchi alisema, “Wanaweza kufanya hivyo ila ni mpaka wapate vibal.”
Kwa mujibu wa maelezo ya wafanyab iashara hao, mayai hayo huuzwa Sh4,000 kwa trei na yanaonekana sio makubwa kama yanayopatikana nchini na yanapovunjwa hayana kiini na baadhi maji yake yamechanganyika na vitu mithili ya nyuzi zenye rangi nyekundu.
Wafanyabiashara hao wanalalamika kuwa kuingizwa nchini kwa mayai hayo yamevuruga soko la ndani ambalo trei moja ilikuwa inauzwa kwa Sh7,000 lakini hayo yanauzwa Sh4,000.
Mayai hayo yanapatikana kwa wingi maeneo ya Kariakoo na Gongo la Mboto na yanauzwa kwa wingi kwa wafanyabiashara wa vyakula jijini Dar es Salaam. Akizungumza na gazeti hili, Mwenyekiti wa Muda wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Mayai Tanzania, Placidia Bambanza alisema mayai hayo yalianza kuingia nchini tangu mwanzoni mwa mwaka huu.
“Tumepanga kupeleka malalamiko yetu kesho (jumatatu) kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na tayari tumeandaa baadhi ya mayai hayo tumuonyeshe na atambue ubovu wake,” alisema Bambanza.
Alisema kuwa hali hiyo imewafanya nao waanze kuuza mayai kwa Sh5000 badala ya Sh7000, jambo ambalo alisema kuwa linawafanya wapate hasara kubwa.
“Tuligundua kuwa mayai haya yanatoka Kenya kwa kuwa wateja wetu ambao awali tulikuwa tukiwauzia mayai, hivi sasa hawanunui kwetu na wanatueleza kuwa wananunua mayai hayo kwa wafanyabiashara kutoka Kenya,” Aliongeza, “Wanatueleza wazi kuwa mayai hayo yanauzika kwa wafanyabiashara wa vyakula kwa kuwa si rahisi kuonekana na watumiaji kama yana kasoro, ila kwa watu ambao hununua mayai kwa ajili ya kuwauzia watu wengine, huyakataa mayai hayo kwa sababu hayauziki na baadhi ya watu wameanza kuyagundua hayafai.”
Alisisitiza kuwa uingizwaji wa mayai hayo nchini unawapa wakati mgumu kwa kuwa wengi wao wamechukua mikopo katika benki mbalimbali nchini, hivyo kitendo cha kuuza trei moja kwa Sh 5000 kinawafanya wapate hasara. Mmoja wa wafanyabiasha hao, Mseti Marwa alisema; “Kama serikali imeruhusu mayai haya yaingie nchini basi wote tuuze bei moja, pia kama wafanyabiashara hawa wana kibali cha kuuza bidhaa hii basi serikali inatakiwa kushusha viwango vya bei za vyakula vya kuku na dawa ili tuweze kuuza kwa bei inayofanana”.
Katika hatua nyingine wafanyabishara hao walilalamikia kampuni za kuuza vifaranga nchini kutokana na vifaranga hivyo kutokuwa na ubora unaotakiwa. “Unaweza kukuta unanunua vifaranga 500 lakini vinatoa mayai trei nane hadi saba tu kitu ambacho si cha kawaida…, katika malalamiko yetu tutaitaka serikali ituruhusu tununue vifaranga kutoka nje ya nchi,” alisema Bambanza Kauli ya serikali Akizungumzia suala hilo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo alisema kuwa yuko tayari kuyapokea malalamiko ya wafanyabiashara hao na kuyafanyia kazi.
“Hilo jambo ndio kwanza nalisikia kutoka kwao… Ila serikali ipo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa soko la ndani linaimarika hivyo nawasubiri ili nisikilize malalamiko yao na nitayafanyia kazi,” alisema Dk Mathayo. Akizungumzia suala la wafanyabiashara kununua vifaranga nje ya nchi alisema, “Wanaweza kufanya hivyo ila ni mpaka wapate vibal.”
Hospitali ya Mount Meru yadaiwa kuua mjamzito
HOSPITALI ya Mkoa wa Arusha Mount Meru imeingia kwenye kashfa baada ya baadhi ya madaktari wake na wauguzi kutuhumiwa kusababisha kifo cha mjamzito ,Florence Joseph (34) mkazi wa Sokoni one jijini Arusha.
Mwili wa marehemu huyo pamoja na kichanga chake tayari imezikwa juzi katika makaburi ya Njiro yaliyopo nje kidogo ya Jiji la Arusha.
Mganga mkuu wa hospitali hiyo,Dk Omar Chande alipohojiwa kuhusu tukio hilo alisema kwamba bado hajapokea taarifa hiyo, lakini aliahidi kufuatilia kwa kina kabla ya kutoa ufafanuzi wa kina.
Akisimulia kisa hicho jirani wa wa marehemu, aliyejitambulisha kwa jina la Katrina Kimaro katika eneo la msiba huo alisema kwamba Febuari 19, mwaka huu saa 10.00 jioni alimsindikiza marehemu kujifungua katika Hospitali ya Levolosi iliyopo jijini hapa baada ya kushikwa na uchungu mkali.
Alisema kwamba mara baada ya kufika hospitalini hapo madaktari katika hospitali hiyo walimpima na kisha kushauri apelekwe haraka Hospitali ya Mount Meru kutokana na kuona njia ya kujifungua ikiwa ndogo.
Katrina, alisema kwamba walifika katika hospitali hiyo saa 12.00 jioni ambapo moja kwa moja waliwasili eneo la mapokezi na kuambiwa wasubiri watahudumiwa lakini cha ajabu kila daktari aliyekuwa akipita eneo hilo alikuwa akiwashangaa.
Alisema kwamba wakati wanaendelea kusubiri katika eneo la mapokezi hospitalini hapo marehemu alikuwa akilalamika mara kwa mara kwamba anasikia uchungu mkali ndipo alipowafuata wauguzi waliokuwapo katika chumba cha mapokezi lakini walimjibu wana shughuli nyingi zinazowaingizia pesa.
“Tulipokuwa eneo la mapokezi marehemu alikuwa akijisikia uchungu mkali kila mara analalamika ikabidi mimi niwafuate wauguzi niwaeleze lakini cha ajabu walinijibu kwamba wana kazi zingine, wanakula vichwa” alisema Kimaro.
Aliendelea kusimulia kisa hicho kwamba ilipofika saa 2.00 usiku alijitokeza daktari mmojawapo aliyewauliza shida yao na ndipo walipomweleza ambapo alifanya taratibu za marehemu kufikishwa katika chumba cha kuzalia na wao waliambiwa warudi nyumbani marehemu atahudumiwa.
Alisema kwamba kesho yake Febuari 20, alfajiri saa 11.00 alifika hospitalini hapo kujua hali ya marehemu endapo ameshajifungua au la na ndipo alipoenda moja kwa moja katika wodi ya wazazi hospitalini hapo na kumtafuta bila mafanikio.
Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipokwenda katika ofisi za chumba cha kuzalia na kumkuta muuguzi mmojawapo na kumwulizia marehemu, lakini cha ajabu muuguzi huyo alitokomea bila kumpa jibu lolote na ndipo alipoamua kwenda katika lango kuu la hospitali hiyo kumwuliza askari aliyekuwa akilinda langoni hapo.
Kimaro, alibainisha kwamba askari huyo alimchukua na kisha kumfikisha kwa muuguzi mwingine waliyemkuta katika wodi ya wazazi akifanya usafi ambapo baada ya kumwelezea shida yake cha ajabu aliwajibu kwamba ametingwa na hawezi kuacha kufanya usafi ashughulikie suala lao.
Alidai baada ya hali hiyo ndipo alipojitokeza daktari mmojawapo baada ya kumwona akihangaika na alipomweleza shida yake akampeleka kwa muuguzi mmojawapo ambaye yuko katika ofisi za chumba cha kuzalia na alipomweleza shida yake alimjibu kwamba wanasikitika mgonjwa wake alifariki jana katika mazingira ya kutatanisha.
Kimaro alisema kwamba muuguzi huyo alimpa maelezo kwamba ilipofika saa 6.00 usiku jopo la madaktari walienda kumchunguza marehemu endapo njia ya kujifungulia imefunguka na ndipo walipompa muda saa moja na kisha kurudi tena saa 7.00 usiku ambapo walimchukua kwa lengo la kwenda kumfanyia upasuaji lakini tayari alikuwa ameshafariki dunia.
“Nakumbuka yule muuguzi alinieleza kwamba ilipofika saa sita usiku walishuka katika chumba cha kuzalia lakini wakamkuta marehemu ana uchungu mkali na njia haijafunguka ndipo walipompa saa moja tena wakarudi saa saba na kuamua kumchukua kumpeleka kumfanyia upasuaji lakini tayari walimkuta marehemu alikuwa ameshakata roho”alisema kwa uchungu
Naye, mume wa marehemu huyo ,Rashid Aloyce alilalamikia kifo cha marehemu mke wake na mtoto kwamba kimetokana na uzembe wa madaktari hospitalini hapo kwa kuwa walimwacha kwa muda wa saa saba bila kumpatia huduma yoyote pamoja na kushikwa uchungu mkali.
Mwili wa marehemu huyo pamoja na kichanga chake tayari imezikwa juzi katika makaburi ya Njiro yaliyopo nje kidogo ya Jiji la Arusha.
Mganga mkuu wa hospitali hiyo,Dk Omar Chande alipohojiwa kuhusu tukio hilo alisema kwamba bado hajapokea taarifa hiyo, lakini aliahidi kufuatilia kwa kina kabla ya kutoa ufafanuzi wa kina.
Akisimulia kisa hicho jirani wa wa marehemu, aliyejitambulisha kwa jina la Katrina Kimaro katika eneo la msiba huo alisema kwamba Febuari 19, mwaka huu saa 10.00 jioni alimsindikiza marehemu kujifungua katika Hospitali ya Levolosi iliyopo jijini hapa baada ya kushikwa na uchungu mkali.
Alisema kwamba mara baada ya kufika hospitalini hapo madaktari katika hospitali hiyo walimpima na kisha kushauri apelekwe haraka Hospitali ya Mount Meru kutokana na kuona njia ya kujifungua ikiwa ndogo.
Katrina, alisema kwamba walifika katika hospitali hiyo saa 12.00 jioni ambapo moja kwa moja waliwasili eneo la mapokezi na kuambiwa wasubiri watahudumiwa lakini cha ajabu kila daktari aliyekuwa akipita eneo hilo alikuwa akiwashangaa.
Alisema kwamba wakati wanaendelea kusubiri katika eneo la mapokezi hospitalini hapo marehemu alikuwa akilalamika mara kwa mara kwamba anasikia uchungu mkali ndipo alipowafuata wauguzi waliokuwapo katika chumba cha mapokezi lakini walimjibu wana shughuli nyingi zinazowaingizia pesa.
“Tulipokuwa eneo la mapokezi marehemu alikuwa akijisikia uchungu mkali kila mara analalamika ikabidi mimi niwafuate wauguzi niwaeleze lakini cha ajabu walinijibu kwamba wana kazi zingine, wanakula vichwa” alisema Kimaro.
Aliendelea kusimulia kisa hicho kwamba ilipofika saa 2.00 usiku alijitokeza daktari mmojawapo aliyewauliza shida yao na ndipo walipomweleza ambapo alifanya taratibu za marehemu kufikishwa katika chumba cha kuzalia na wao waliambiwa warudi nyumbani marehemu atahudumiwa.
Alisema kwamba kesho yake Febuari 20, alfajiri saa 11.00 alifika hospitalini hapo kujua hali ya marehemu endapo ameshajifungua au la na ndipo alipoenda moja kwa moja katika wodi ya wazazi hospitalini hapo na kumtafuta bila mafanikio.
Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipokwenda katika ofisi za chumba cha kuzalia na kumkuta muuguzi mmojawapo na kumwulizia marehemu, lakini cha ajabu muuguzi huyo alitokomea bila kumpa jibu lolote na ndipo alipoamua kwenda katika lango kuu la hospitali hiyo kumwuliza askari aliyekuwa akilinda langoni hapo.
Kimaro, alibainisha kwamba askari huyo alimchukua na kisha kumfikisha kwa muuguzi mwingine waliyemkuta katika wodi ya wazazi akifanya usafi ambapo baada ya kumwelezea shida yake cha ajabu aliwajibu kwamba ametingwa na hawezi kuacha kufanya usafi ashughulikie suala lao.
Alidai baada ya hali hiyo ndipo alipojitokeza daktari mmojawapo baada ya kumwona akihangaika na alipomweleza shida yake akampeleka kwa muuguzi mmojawapo ambaye yuko katika ofisi za chumba cha kuzalia na alipomweleza shida yake alimjibu kwamba wanasikitika mgonjwa wake alifariki jana katika mazingira ya kutatanisha.
Kimaro alisema kwamba muuguzi huyo alimpa maelezo kwamba ilipofika saa 6.00 usiku jopo la madaktari walienda kumchunguza marehemu endapo njia ya kujifungulia imefunguka na ndipo walipompa muda saa moja na kisha kurudi tena saa 7.00 usiku ambapo walimchukua kwa lengo la kwenda kumfanyia upasuaji lakini tayari alikuwa ameshafariki dunia.
“Nakumbuka yule muuguzi alinieleza kwamba ilipofika saa sita usiku walishuka katika chumba cha kuzalia lakini wakamkuta marehemu ana uchungu mkali na njia haijafunguka ndipo walipompa saa moja tena wakarudi saa saba na kuamua kumchukua kumpeleka kumfanyia upasuaji lakini tayari walimkuta marehemu alikuwa ameshakata roho”alisema kwa uchungu
Naye, mume wa marehemu huyo ,Rashid Aloyce alilalamikia kifo cha marehemu mke wake na mtoto kwamba kimetokana na uzembe wa madaktari hospitalini hapo kwa kuwa walimwacha kwa muda wa saa saba bila kumpatia huduma yoyote pamoja na kushikwa uchungu mkali.
Giggs mkongwe aliyecheza mechi 900 Man. United
LONDON, England
KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amempongeza mkongwe wake, Ryan Giggs akisema ni kati ya wachezaji wanaozeeka huku kiwango cha soka kikiwa bado juu.
Giggs, 38, ambaye amecheza mechi 900 za United kaika mashindano yote, ni kati ya wachezaji wanaotarajiwa kupewa heshima katika klabu hiyo kwa utumishi wa muda mrefu.
Hiyo itamfanya Giggs kuendelea kuuwania ubingwa ikiwa ni pamoja na kuwa miongoni mwa wachezaji wa pambano la Norwich lililopigwa jana na Ferguson anaamini kuwa hakuna mchezaji kama yeye.
"Kwa mtazamo wangu, na siamini kama kila mmoja atakubaliana na mimi, kuwemo kwenye Ligi Kuu na licha ya kufaya makubwa, siamini kama kuna mchezaji mwingine anaweza kumfikia," anasema kocha wa United juzi.
"Pamoja na ukongwe wake, anajaribu kutengeneza mazingira mazuri kufanikisha azma ya uchezaji wake. Anacheza kiwango cha juu, na leo, anacheza kama wachezaji wengine. Anafurahisha."
Ferguson anaamini kuwa kujituma, kujitunza na kufuata taratibu za mchezo ndicho kilichomfanya Giggs kucheza kwa muda mrefu.
"Giggs ni kati ya wachezaji waliokomaa, amekuwa akikimbiza vizuri na zaidi hupenda kusimama namba za katikati ya dimba la mbele. Huopewa nafasi kama mchezaji wa kipekee kwenye timu," anasema.
"Itakumbukwa Ryan a mekuwa mchezaji mashuhuri kwa kupanda na kushuka na mch ezaji makini sana anapokuwa uwanjani.
"Amekuwa akibadilika sana na amekuwa akibadilika tofauti na ilivyokuwa miaka 10 iliyopita na anapokuwa mchezoni anaonekana tofauti na unavyomdhania."
Giggs ameingia mkataba wa mwaka mmoja, utakaomfanya abaki Old Trafford hadi mwisho wa msimu wa 2013 na, pia amecheza mechi 64 na timu ya taifa ya Wales na mbili za U-21 na lengo lake ni kufikisha mechi 1,000 kabla ya kustaafu soka.
"Juu ya umri," Ferguson, anasema kuwa hilo linawezekana.
"Stanley Matthews amecheza soka akiwa na miaka 50, tusubiri kwa Giggs na tuone."
*Maisha ya Giggs
Ryan Joseph Wilson ni mtoto wa kufikia aliyelelewa katika kituo cha St David's Hospital mjini Canton, Cardiff, cha Danny Wilson,
Akiwa na umri mdogo Giggs amekulia katika eneo la Ely, magharibi mwa Cardiff. Mdogo wake, Rhodri, alikuwa akiichezea klabu ya Salford City.
Ametumia muda mwingi kucheza barabarani na watoto wenzake kwenye mji wa Pentrebane. Mwaka 1980, Giggs akiwa na miaka sita, alisaini Swinton RLFC, na familia nzima ikahamia Swinton, katika mji wa Salford, Greater Manchester.
Mwaka 1990-1995, alianza kuichezea Manchesster United kwani alipewa mkataba Novemba 29, 1990 (akiwa na miaka 17). Alianza kucheza soka kama mwanasoka wa kulipwa (1 Desemba 1990).
Akiwa na timu hiyo kombe lake la kwanza lilikuwa FA na kimsingi Giggs alianza kuichezea timu yake dhidi ya Everton kwenye Uwanja wa Old Trafford Machi 2, 1991 akitokea benchi kuchukua nafasi ya Denis Irwin.
Giggs alianza kuichezea timu ya kwanza akiwa na miaka 17, na kuweka rekodi yake kuwa mchezaji mwenye umri mdogo kuitumikia Manchester United. Huo ukawa mwanzo wa kuitumikia klabu ya wakubwa ya Ferguson
KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amempongeza mkongwe wake, Ryan Giggs akisema ni kati ya wachezaji wanaozeeka huku kiwango cha soka kikiwa bado juu.
Giggs, 38, ambaye amecheza mechi 900 za United kaika mashindano yote, ni kati ya wachezaji wanaotarajiwa kupewa heshima katika klabu hiyo kwa utumishi wa muda mrefu.
Hiyo itamfanya Giggs kuendelea kuuwania ubingwa ikiwa ni pamoja na kuwa miongoni mwa wachezaji wa pambano la Norwich lililopigwa jana na Ferguson anaamini kuwa hakuna mchezaji kama yeye.
"Kwa mtazamo wangu, na siamini kama kila mmoja atakubaliana na mimi, kuwemo kwenye Ligi Kuu na licha ya kufaya makubwa, siamini kama kuna mchezaji mwingine anaweza kumfikia," anasema kocha wa United juzi.
"Pamoja na ukongwe wake, anajaribu kutengeneza mazingira mazuri kufanikisha azma ya uchezaji wake. Anacheza kiwango cha juu, na leo, anacheza kama wachezaji wengine. Anafurahisha."
Ferguson anaamini kuwa kujituma, kujitunza na kufuata taratibu za mchezo ndicho kilichomfanya Giggs kucheza kwa muda mrefu.
"Giggs ni kati ya wachezaji waliokomaa, amekuwa akikimbiza vizuri na zaidi hupenda kusimama namba za katikati ya dimba la mbele. Huopewa nafasi kama mchezaji wa kipekee kwenye timu," anasema.
"Itakumbukwa Ryan a mekuwa mchezaji mashuhuri kwa kupanda na kushuka na mch ezaji makini sana anapokuwa uwanjani.
"Amekuwa akibadilika sana na amekuwa akibadilika tofauti na ilivyokuwa miaka 10 iliyopita na anapokuwa mchezoni anaonekana tofauti na unavyomdhania."
Giggs ameingia mkataba wa mwaka mmoja, utakaomfanya abaki Old Trafford hadi mwisho wa msimu wa 2013 na, pia amecheza mechi 64 na timu ya taifa ya Wales na mbili za U-21 na lengo lake ni kufikisha mechi 1,000 kabla ya kustaafu soka.
"Juu ya umri," Ferguson, anasema kuwa hilo linawezekana.
"Stanley Matthews amecheza soka akiwa na miaka 50, tusubiri kwa Giggs na tuone."
*Maisha ya Giggs
Ryan Joseph Wilson ni mtoto wa kufikia aliyelelewa katika kituo cha St David's Hospital mjini Canton, Cardiff, cha Danny Wilson,
Akiwa na umri mdogo Giggs amekulia katika eneo la Ely, magharibi mwa Cardiff. Mdogo wake, Rhodri, alikuwa akiichezea klabu ya Salford City.
Ametumia muda mwingi kucheza barabarani na watoto wenzake kwenye mji wa Pentrebane. Mwaka 1980, Giggs akiwa na miaka sita, alisaini Swinton RLFC, na familia nzima ikahamia Swinton, katika mji wa Salford, Greater Manchester.
Mwaka 1990-1995, alianza kuichezea Manchesster United kwani alipewa mkataba Novemba 29, 1990 (akiwa na miaka 17). Alianza kucheza soka kama mwanasoka wa kulipwa (1 Desemba 1990).
Akiwa na timu hiyo kombe lake la kwanza lilikuwa FA na kimsingi Giggs alianza kuichezea timu yake dhidi ya Everton kwenye Uwanja wa Old Trafford Machi 2, 1991 akitokea benchi kuchukua nafasi ya Denis Irwin.
Giggs alianza kuichezea timu ya kwanza akiwa na miaka 17, na kuweka rekodi yake kuwa mchezaji mwenye umri mdogo kuitumikia Manchester United. Huo ukawa mwanzo wa kuitumikia klabu ya wakubwa ya Ferguson
Arsenal yaingia mwaka wa saba bila ubingwa
LONDON, England
WIKI mbili zilizopita, zilikuwa mbaya kwa mashabiki wa Arsenal. Katika kipindi cha siku nne, the Gunners ilichapwa na AC Milan 4-0, na kuififisha nafasi ya Arsenal kuendelea na Ligi ya Mabingwa Ulaya. Na Jumamosi Februari, 18, Sunderland iliwaliza Gunners 2-0.
Kwa hali hiyo, inafanya kikosi cha Arsene Wenger kumaliza msimu wa saba bila ubingwa na zaidi ni baada ya kufungwa mechi ya Sunderland.
Arsenal inatakiwa kufanya mabadiliko makubwa na zaidi katika kutengeneza kikosi cha kwanza kwanza. Kwa mujibu wa Sunday Mirror, miongoni mwa watu wa ngazi za juu wa Gunners kuna haja ya kufanyia mabadiliko safu nzima ya timu.
Manchester City imeanza kuiga staili ya Arsenal kwani imeanza kutengeneza wachezaji chipukizi. Cha kushangaza, Wenger na uongozi mzima wa Arsenal wanashindwa kutoka kupitia mazao ya chipukizi wao.
Mpango wa sasa ni kumpatia Wenger uwezo wa kusajili wachezaji wakubwa na kuongeza mishahara kwa wachezaji waliopo, Robin van Persie, Arsenal ni miongoni mwa wachezaji watakaoneemeka.
Robin van Persie amebakisha mwaka mmoja kumaliza mkataba wake na Arsenal. Bosi ya klabu kwa sasa inazungumza na Wenger kwa ajili ya kununua wachezaji wakubwa kuibeba klabu.
Baadhi wameanza kusema kuwa hali ni mbaya kwa sasa Arsenal katika historia ya uongozi wake na kwamba mechi mbili zilizopita, zimekuwa tatizo.
Ni wakati kwa Arsenal kufanya maamuzi magumu. Inatakiwa kutengeneza timu kutoka uwanjani hadi kwa wachezaji mmoja mmoja kwani vinginevyo mashabiki wanaweza wasinunue ama kubakia vyooni wakiangalia kupitia kwenye televisheni.
WIKI mbili zilizopita, zilikuwa mbaya kwa mashabiki wa Arsenal. Katika kipindi cha siku nne, the Gunners ilichapwa na AC Milan 4-0, na kuififisha nafasi ya Arsenal kuendelea na Ligi ya Mabingwa Ulaya. Na Jumamosi Februari, 18, Sunderland iliwaliza Gunners 2-0.
Kwa hali hiyo, inafanya kikosi cha Arsene Wenger kumaliza msimu wa saba bila ubingwa na zaidi ni baada ya kufungwa mechi ya Sunderland.
Arsenal inatakiwa kufanya mabadiliko makubwa na zaidi katika kutengeneza kikosi cha kwanza kwanza. Kwa mujibu wa Sunday Mirror, miongoni mwa watu wa ngazi za juu wa Gunners kuna haja ya kufanyia mabadiliko safu nzima ya timu.
Manchester City imeanza kuiga staili ya Arsenal kwani imeanza kutengeneza wachezaji chipukizi. Cha kushangaza, Wenger na uongozi mzima wa Arsenal wanashindwa kutoka kupitia mazao ya chipukizi wao.
Mpango wa sasa ni kumpatia Wenger uwezo wa kusajili wachezaji wakubwa na kuongeza mishahara kwa wachezaji waliopo, Robin van Persie, Arsenal ni miongoni mwa wachezaji watakaoneemeka.
Robin van Persie amebakisha mwaka mmoja kumaliza mkataba wake na Arsenal. Bosi ya klabu kwa sasa inazungumza na Wenger kwa ajili ya kununua wachezaji wakubwa kuibeba klabu.
Baadhi wameanza kusema kuwa hali ni mbaya kwa sasa Arsenal katika historia ya uongozi wake na kwamba mechi mbili zilizopita, zimekuwa tatizo.
Ni wakati kwa Arsenal kufanya maamuzi magumu. Inatakiwa kutengeneza timu kutoka uwanjani hadi kwa wachezaji mmoja mmoja kwani vinginevyo mashabiki wanaweza wasinunue ama kubakia vyooni wakiangalia kupitia kwenye televisheni.
Chelsea yachanja...
LONDON, England
CHELSEA imeendelea kuchanja mbuga baada ya kuibandua Bolton mabao 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya England na kumaliza ukame wa ushindi wa timu hiyo wa mechi tano mfululizo.
Bolton iliyokuwa imeikaba Blues lakini kabla ya mapumziko, Mbrazil, David Luiz alitupia mpira ndani ya kimia kuandika bao la kwanza kwa timu yake.
Didier Drogba alipiga kichwa cha karibu na kufanya matokeo kuwa 2-0 kabla ya Frank Lampard kumalizia krosi ya Juan Mata.
Wageni walipoteza nafasi baada ya Ryo Miyaichi kukosa bao la wazi ambalo lingewafanya kuwa mbele kabla ya Chelsea kufunga. Chelsea imefikisha pointi 46 na kuishusha Arsenal ambayo jana ilikuwa na kazi dhidi ya Tottenham.
Mechi nyingine za jana usiku, Norwich ilikuwa ikicheza na Man United huku Stoke ikiikaribisha Swansea.
Mbali na mechi hizo, West Brom iliyokuwa nyumbani hiyo juzi, iliitandika Sunderland mabao 4-0. Sunderland iliifunga Arsenal katika moja ya mechi za ligi hiyo hivi karibuni.
Nayo QPR ilishindwa kutumia uwanja wa nyumbani na kuchapwa bao 1-0 na Fulham wakati Newcastle ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 2-2 na Wolves. Wigan na Aston Villa zenyewe zilitoka suluhu katika mfululizo wa mechi hizo.
CHELSEA imeendelea kuchanja mbuga baada ya kuibandua Bolton mabao 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya England na kumaliza ukame wa ushindi wa timu hiyo wa mechi tano mfululizo.
Bolton iliyokuwa imeikaba Blues lakini kabla ya mapumziko, Mbrazil, David Luiz alitupia mpira ndani ya kimia kuandika bao la kwanza kwa timu yake.
Didier Drogba alipiga kichwa cha karibu na kufanya matokeo kuwa 2-0 kabla ya Frank Lampard kumalizia krosi ya Juan Mata.
Wageni walipoteza nafasi baada ya Ryo Miyaichi kukosa bao la wazi ambalo lingewafanya kuwa mbele kabla ya Chelsea kufunga. Chelsea imefikisha pointi 46 na kuishusha Arsenal ambayo jana ilikuwa na kazi dhidi ya Tottenham.
Mechi nyingine za jana usiku, Norwich ilikuwa ikicheza na Man United huku Stoke ikiikaribisha Swansea.
Mbali na mechi hizo, West Brom iliyokuwa nyumbani hiyo juzi, iliitandika Sunderland mabao 4-0. Sunderland iliifunga Arsenal katika moja ya mechi za ligi hiyo hivi karibuni.
Nayo QPR ilishindwa kutumia uwanja wa nyumbani na kuchapwa bao 1-0 na Fulham wakati Newcastle ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 2-2 na Wolves. Wigan na Aston Villa zenyewe zilitoka suluhu katika mfululizo wa mechi hizo.
Watanzania wachemka Kili Marathon
Wanariadha wa Kenya, Ezekiel Kimath (kushoto) Kimot Chemo na David Kipromo, wakiongoza mbio za Kilimanjaro Marathon zilizofanyika mjini Moshi jana. Wanariadha hao walitamba kwa kuchukua nafasi zote 20 za juu kwa upande wa wanaume na wanawake. Picha na Mussa Zumba.
TANZANIA imeendelea kuwa msindikizaji katika medani ya kimataifa baada ya wanariadha wake pekee, Fabian Joseph kushika nafasi ya tatu kwa upande wa wanaume na Mary Naali kushika nafasi ya tano kwa upande wa wanawake katika mbio za Kilimanjaro Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Wakati hali ikiwa mbaya kwa wanariadha wa Tanzania, Kenya imeendelea kutawala mbio hizo baada ya wanariadha wake (wanaume kwa wanawake) kukamata nafasi zote tatu muhimu za juu katika mbio za Kilometa 42 za Kilimanjaro Premium Lager na Nusu Marathon Kilometa 21.
Katika mbio hizo, Joseph alikamata nafasi ya tatu katika mbio za nusu marathon kwa upande wa wanaume baada ya kutumia saa 1:03:32 na kuzawadiwa medali ya shaba wakati Naali alikamata nafasi ya tano katika mbio za nusu marathon baada ya kutumia saa 1:15:47 kwa upande wa wanawake.
Umahiri wa Wakenya ulianzia katika mbio za Kilimanjaro Marathon za Kilometa 42 kwa upande wa wanaume, ambapo David Kipron aliibuka mshindi wa kwanza baada ya kutumia saa 2:13:57, wakati Ezekil Kimtai alikamata nafasi ya pili baada ya kutumia saa 2:14:06 huku Kibeth Timoth akimaliza mshindi wa tatu kwa kutumia saa 2:15:38.
Uhodari huo wa Wakenya hao uliendelea kwa upande wa wanawake ambapo Monica Jopkoech alimaliza mshindi wa kwanza baada ya kutumia saa 2:42:45 wakati Peris Jepkorir alishika nafasi ya pili baada ya kutumia saa 2:43:02 na Panuelag Anesomi alitwaa nafasi ya tatu akitumia saa 2:43:41.
Katika mbio za nusu marathon, Hosea Mallel aliendeleza wimbi la ushindi kwa Wakenya alipotumia saa 1:03:00 na kuibuka mshindi kwa upande wa wanaume, wakati Ngengi Jofrey alikamata nafasi ya pili baada ya kutumia saa 1:03:32 na kumwacha Mtanzania Joseph akikamata nafasi ya tatu alipotumia saa 1:03:14.
Naye Vicoty Chepkemoi alikuwa mbabe kwa upande wa wanawake alipoibuka mshindi wa kwanza baada ya kutumia saa 1:13:00, huku Wakenya wenzake Cythia Limo akikamata nafasi ya pili baada ya kutumia saa 1:13:07 na Flomena Daniel aliyemaliza akiwa katika nafasi ya tatu baada ya kutumia saa 1:14:48.
Kivumbi kingine kilikuwa katika mbio za kujifurahisha, ambapo Gareth Ismail aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume wakati Brazil Boy alishika nafasi ya pili na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Fabia Nelson wakati ambapo Jaquline Juma aliibuka mshindi wa mbio hizo kwa upande wa wanawake, akimwacha Catherine Yuko katika nafasi ya pili na Nathaniel Elisante aliyemaliza katika nafasi ya tatu.
Washindi wa kwanza wa mbio za Kilimanjaro Marathon (wanawake na wanaume) walizawadiwa Sh 6 milioni, Sh 3 kwa washindi wa pili na 1,500,000 kwa washindi wa tatu,huku zawadi hizo zikiendelea katika mtitiriko wake.
Naye mshindi wa pili wa mbio za nusu marathon (wanaume kwa wanawake) walizawadiwa Sh 3 milioni, mshindi wa pili Sh 1,500,000 na mshindi wa tatu Sh 750,000 kwa mtiririko wake huku washindi wa mbio nyingine kama za kujifurahisha na Gapco pia walipata zawadi mbalimbali ikiwamo fedha taslimu.
Subscribe to:
Comments (Atom)







